Nafasi za kazi katika Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi

General Description

Source: Utumishi Zanzibar



Release date: 2019-04-08



Duty Station: Zanzibar
16698 visits!... Deadline: 2019-04-12 15:30:00

Tume ya Utumishi Serikalini inatangaza nafasi za kazi katika Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kama ifuatavyo:- 

1. Mpishi Mkuu Daraja la II “Nafasi 1” Unguja 

Sifa za Waombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu Shahada ya Kwanza katika fani ya Ukarimu na Usimamizi wa Mambo ya Utalii na Uzoefu wa kazi ya Upishi usiopunguwa miaka (8) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 



2.Msaidizi Mpishi Mkuu Daraja la III “Nafasi 1” Unguja 

Sifa za Waombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu elimu ya Stashahada katika fani ya Ukarimu na Usimamizi wa Mambo ya Utalii na Uzoefu wa kazi ya Upishi usiopunguwa miaka (5) kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 


3.Wapishi Daraja la III “Nafasi 2” Unguja na 2” Pemba 

Sifa za Waombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu elimu ya Stashahada katika fani ya Ukarimu na Usimamizi wa Mambo ya Utalii kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 



4.Wahudumu Daraja la III “Nafasi 4” Unguja na 6” Pemba 

Sifa za Waombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amemaliza elimu ya Sekondari. 



5.Fundi Magari Daraja la III “Nafasi 1” Unguja 


Sifa za Waombaji: 
•Awe ni Mzanzibari. 
•Awe amehitimu elimu ya Cheti katika fani ya Ufundi Magari kutoka katika Chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. 




Jinsi ya Kuomba: 
•Barua za maombi ziandikwe kwa Mkono na zitumwe kwa anuani ifuatayo:- 



KATIBU, 
TUME YA UTUMISHI SERIKALINI, 
S. L. P 1587 - ZANZIBAR. 

•Muombaji anaombwa kuwasilisha ombi lake moja kwa moja katika Ofisi ya Tume ya Utumishi Serikalini iliyopo Jumba la Wananchi Forodhani Zanzibar wakati wa saa za kazi. Kwa waombaji walioko Pemba wanaombwa kuwasilisha maombi yao Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Chake Chake Pemba. Muombaji anatakiwa kuainisha nafasi anayoiomba vyenginevyo maombi yake hayatazingatiwa. 

Barua za Maombi ziambatanishwe na mambo yafuatayo:- 
a) Kivuli cha Cheti cha kumalizia masomo 
b) Kivuli cha Cheti cha mtihani wa Taifa (Elimu ya Sekondari) 
c) Kivuli cha Cheti cha Kuzaliwa. 
d) Kivuli cha Kitambulisho cha Mzanzibari. 
e) Picha moja (1) ya Passport Size iliyopigwa karibuni. 
f) N.B: Atakaewasilisha ‘Statement of Result’ au ‘Progressive Report’ maombi yake hayatazingatiwa. 
g) Tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ni tarehe 12 Aprili, 2019 wakati wa saa za kazi. 



Share via Whatsapp

Others

Promoted Ads

No preview available
Highheels
1149

Visits

TZS 25,000
No preview available
Dishdash
875

Visits

TZS 20,000
No preview available
Night dress
992

Visits

TZS 8,000
No preview available
saa za kike
1187

Visits

TZS 15,000
No preview available
vyetezo vya umeme
959

Visits

TZS 10,000
No preview available
maua
976

Visits

TZS 7,000
No preview available
bulb
654

Visits

TZS 3,000

+ Tafadhali weka maoni yako hapa..

Advertise with us

© 2025 Zenji Shoppazz . All rights reserved | Design by W3layouts and Zenji Shoppazz Choose language : Kiswahili